Msanii wa mziki wa kizazi kipya Gentriez Mwakitabu kutoka label ya mziki ya Wanene Ent yenye makao yake makuu mjini Arusha, kupitia account yake katika mtandao wa kijamii wa Facebook ameelezea kusikitishwa kwake na ubunifu mdogo unaofanywa na wasanii wa hapa Bongo katika kazi zao.
Gentriez akionesha kulalama kutokana na kutumiwa kwa jina la Album yake pamoja na Idea ya video ameandika
'NIMEIBIWA jina la album yangu ya chumba cha mtihani pamoja na idea ya video yangu ya Kila sababu.. huyo jamaa anaitwa nzige. Audio ameifanya kwa maneke na amemshirikisha noorah. Huo sio ubunifu hata kidogo...#wanene'
No comments: