728x90 AdSpace

MPYA

[recent][ticker2]
13 May 2012

Stanboi Jukwaa Moja na Sean Paul

Ni show ya mkali wa Dancehall na kipenzi cha masista duu, Sean Paul kutoka Kingston,Jamaica itakayofanyika May 17, Wichita,Kansas nchini Marekani.Tamasha hili lina faraja pia kwa wapenzi wa muziki wa Tanzania. Ni katika show hiyo kijana mwenye kipaji kutoka Bongo ambaye si mgeni kwa wengi atashare stage moja na mkali huyo.Si mwingine ni Stanboi aka the African Child.Kupanda stage moja na Sean Paul si kitu rahisi kama CV yako inachechemea. Lakini pia mjini Wichita kuna wakali wengine hivyo swali ni kwamba Stanboi amepataje shavu hili?
Akizungumzia hilo Stanboi amesema sio mara ya kwanza kutumbuiza katika show kama hizo na wasanii wakubwa kwani moja ya station za Radio huko Kansas (Power 93.9) huandaa show zote kubwa hivyo pia kutokana na kuwa wanacheza nyimbo zake huwa wanampa nafasi!
Stanboi alifunguka furaha aliyonayo ku share stage moja na Sean Paul akikiri kwamba nafasi kama hizo huwa haziji kiurahisi!
Stanboi moja kati ya wasanii wachache wanaoiwakilisha vyema Tanzania nje ameshawahi fanya show na wasanii kama Mims, Chamilionare, Baby Bash, Kreayshawn na wengine kibao!!

Nolniz wish you:
All tha best Broda & endelea kutuwakilisha vyema

©2012 Nolniz Blog™
Stanboi Jukwaa Moja na Sean Paul Reviewed by Nolniz on Sunday, May 13, 2012 Rating: 5 Ni show ya mkali wa Dancehall na kipenzi cha masista duu, Sean Paul kutoka Kingston,Jamaica itakayofanyika May 17, Wichita,Kansas nchini Mar...

[][carousel1]

No comments: